Twen'zetu Bungoma Bwanaa!

Tuma Ikisiri Sasa

Twen'zetu Bungoma 2025

14 Disemba, 2025
Chuo Kikuu cha Kibabii, Bungoma Kenya
Tukakongamaneni

Kuhusu Kongamano Hili​

Kuhusu Kongamano Hili​

Kutana na wataalamu, wakereketwa, na wadau wa Kiswahili toka sehemu mbalimbali Duniani. Utafurahi kutangamana na Waswahili wengine na kuwa sehemu ya familia kubwa ya wasemaji wa Kiswahili Duniani! Mada kuu ni “Mnasaba wa Kiswahili na Nyuga Nyingine: Dira ya Mustakabali.” Jioni ya tarehe 16 Disemba, kutakuwa na tamasha kubwa la Utamaduni wa Mswahili, ambapo watu wote wanakaribishwa, hata wale ambao hawakushiriki katika kongamano.

Kamati ya maandalizi inaangalia uwezekano wa kuandaa shughuli za kitalii zitakazofanyika siku ya Jumatano, Disemba 17. Wale watakaohitaji kushiriki katika utalii watajulishwa gharama zitakuwa kiasi gani na ni maeneo gani ya kiutalii yatakayotembelewa.

Kwanini ushiriki kongamanoni?

Ni kwanini Ushiriki?

Yawezekana unajiuliza swali hili: ni kwanini nishiriki kwenye kongamano hili? Nitapata faida gani?

Jumuika

Kongamano la Kimataifa la CHAUKIDU linakuwa fursa ya kujumuika katika harakati za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili​

Wasemaji Mahiri

Kongamano hili litakupa fursa ya kusikiliza mawasilisho ya mada elekezi kutoka kwa wasemaji mahiri na waliobobea katika fani zao. ​

Pata Marafiki Wapya

Kongamano hili linakupa fursa ya kukutana na watu mbalimbali toka sehemu mbalimbali za dunia. Kutana na watu wapya kongamanoni!​

Tukakongamaneni

Je, umeshajiwekea malazi?

Hoteli na Malazi

Ili kulifurahia kongamano, utahitaji mahali pazuri pa malazi. Kamati-andalizi imewaandalia malazi ndani ya chuo cha MS TCDC na nje karibu na chuo. Japo chaguo ni lako, hakikisha unahifadhi malazi mapema ili upate mahala ambapo utapafurahia zaidi.

Malazi Ndani ya Kibabii

Haya ni malazi ya viwango mbalimbali yapatikanayo ndani ya chuo. Kamati-Andalizi imefanya mazungumzo na idara ya malazi chuoni na kupewa bei za punguzo kwa wakongamanaji. Jihifadhie malazi mapema ili kukwepa usumbufu unaoweza kujitokeza.

Malazi Nje ya Kibabii

Haya ni malazi ya viwango mbalimbali yapatikanayo nje ya chuo. Kamati-Andalizi imefanya mazungumzo na idara ya malazi chuoni na kupewa bei za punguzo kwa wakongamanaji. Jiwekee malazi mapema ili kukwepa usumbufu unaoweza kujitokeza.

Jisajili Sasa!

Harakisha! Watakaojisajili mapema watapata punguzo!​

Wale watakaojisajili mapema, watalipa ada yenye punguzo. Pia, ukiwa mwanachama hai wa CHAUKIDU kwa mwaka huu, unapata punguzo zaidi.

Wasemaji Wetu

Nani ni Wasemaji Wakuu?

Wasemaji mahiri na wenye tajiriba kubwa watashiriki katika kongamano hili. Taarifa zaidi kuhusu wasemaji zitatolewa.

Makala Elekezi

Prof. Profesa

Profesa Profesa
Chuo Kikuu cha
Kenya

Makala Maalumu

Prof. Jina Jina

Profesa wa Isimu ya Afrika
Chuo Kikuu cha
Tanzania

Ratiba Yetu

Ratiba ya Mawasilisho

Ratiba yetu inapatikana hapa.

Ada ya Kongamano

Lipa Ada ya Kongamano

Ada ya kongamano hili ni ndogo, hasa kwa wadau wetu watokao Afrika Mashariki. Lengo letu ni kuwapa fursa wadau wengi kushiriki katika kongamano hili kwa kuondoa vikwazo vya kiuchumi. Ukilipa ada ya kongamano mapema, kabla ya Nov. 01 2023, utapata bei ya punguzo. Chagua kategoria inayokufaa hapo chini.

Ada ya Kongamano - Wanafunzi Wanachama

Conference Registration Student – Members

Ada ya Kongamano - Wanafunzi Wasio Wanachama

Conference Registration – Student Non-Members

Ada ya Kongamano - Kawaida Wasio Wanachama

Conference Registration Regular- Non-Members

Ada ya Kongamano - Kawaida Wanachama

Conference Registration Regular – Members

0 +
Wawasilishaji
0 +
Washiriki
0
Sikuza Kongamano
0 +
Masaa ya Kongamano

Wadhamini

Wadhamini

Kongamano haliwezi kufanikiwa bila kuwa na wadhamini. Ikiwa ungependa kuwa mdhamini wa kongamano la CHAUKIDU, tuandikie nasi tutaweka nembo ya taasisi au biashara yako hapa katika tovuti yetu na kwenye vitabu vyetu vya kongamano.

Wadhamini Wakuu

Utalikosaje?

Usikose Kongamano Lenye Hadhi ya Kidunia

Hili ni kongamano lenye hadhi ya kidunia. Litawaleta wadau kutoka nchi na maeneo mbalimbali duniani. Kuwa sehemu ya familia kubwa ya Waswahili kote ulimwenguni. Usikose!

MAYASA

Maswali Yaulizwayo Sana

Kuna maswali ambayo wadau wetu wanayauliza mara kwa mara. Tafadhali angalia kama swali ulilokuwa nalo limejibiwa humu:

Katika makongamano yote ya CHAUKIDU, ikisiri hutumwa kwa mfumo maalumu wa ikisiri. Mfumo huu huwezesha upokeaji na utathmini wa ikisiri zote. Bofya hapa kutuma ikisiri yako.

Unakuwa mwanachama hai wa CHAUKIDU kwa kulipa ada ya kila mwaka. Lipa ada yako uwe mwanachama hai sasa.

Hapana. CHAUKIDU si chama cha walimu pekee. Ni chama cha wadau na wakereketwa wote wa Kiswahili.

Kumbukumbu

Picha za CHAUKIDU 2022

Hizi ni baadhi ya picha za kongamano letu la mwaka 2022, jijini Washington DC.

[conference_schedule]

Contact Us

Wasiliana Nasi

Ikiwa una swali au maoni kuhusiana na kongamano la kimataifa la CHAUKIDU la 2023, tafadhali wasiliana nasi.

Address

2816 Cathedral of Learning, Pittsburgh, PA 15260

Contact
Email

makongamano@chaukidu.org